Pages

Wednesday, November 30, 2011

what is leadership?




TUIJENGE TANZANIA

TOFAUTI KATI YA NCHI TAJIRI NA MASIKINI SIO KUWA NA UHURU KWA MUDA MREFU.

  • Kwa mfano Ethiopia na Liberia, ambazo hazikutawaliwa barani Africa lakini bado hazijaendelea(maskini).
  • K wa upande mwingine nchi kama Corea, South Africa, Canada na Austaria ambazo zilipata uhuru miaka 150 iliyopita lakini ni nchi zilizoendelea (mf. South ilipata uhuru 1990).

TOFAUTI KATI YA NCHI MASIKINI NA TAJIRI HAIPO KWENYE UPATIKANAJI NA UWEPO WA MALIASIRI.

  • Kwa mfano, Japan ambayo 80% ya eneo lake ni milima na haina eneo la kulima au kufugia mifugo, lakini ni nchi ya tatu duniani kwa utajiri, inaingiza maligafi (raw material) kutoka pande zote za dunia na inazalisha bidhaa( manufactured products) kwenda pande zote za dunia.
  •    mf. mwingine ni Swit zerland, ambayo hailimi cocoa lakini inazalisha chocolate bora duniani. katika eneo lake dogo inafuga mifugo na inalima misimu minne(4) kwa mwaka.

UTOFAUTI UNAKUJA WAPI SASA?

Utofauti ni ile tabia ya watu, walivyojijengea  akilini mwao kutokana na elimu wanayopata na utamaduni wao.

Katika kuzichambua tabia za watu wanaoishi nchi zilizoendelea na tajiri, unafahamu kuwa wao walizingatia haya yafuatayo:-
  1. kujifunza  kuwa kipini kizuri na kipi ni kibaya katika jamii ya mwanadamu. (ethics) hii ilkuwa sheria kubwa walioitumia.
  2. kuwa na matamanio ya mambo makubwa (will of super action).
  3. punctuality.
  4. KUHESHIMU NA KUZIFUATA SHERIA NA KANUNI WALIZO JIWEKEA.
  5. KUFANYA KAZI KWA UPENDO.
  6. KUTEKELEZA MAJUKUMU KWA KILA MMOJA KULINGANANA WADHIFA WAKE.
  7. na KUHESHIMU HAKI ZA KILA MWANANCHI.
Katika nchi masikini ni wachache wanatekeleza hayo katika taratibu zao za kila siku.

WATANZANIA SIO MASIKINI KWA SABABU HATUNA MALIGHAFI.
Watanzania ni masikini kwa sababu hatuna matarajio ya kufanya kitu kikubwa, hatutekelezi majukumu yetu ipasavyo.
KWA UZALENDO WA KUIPENDA NCHI YAKO, WATUMIA MARAFIKI UJUMBE HUU, NAWE PIA UUFUATE ILI TUIBADILISHE TANZANIA.
                                              MUNGU IBARIKI AFRICA
                                MUNGU IBARIKI TANZANIA.

Sunday, November 27, 2011

HELLO FRIEND

Once I sat and thought of what is FRIEND to me???
And I came to a conclusion which I would like to share it with My Near and Friend......
THAT'S U!!!!


It is BY CHANGE we met, BY CHOICE we became friends......

Friendship is a strange thing....

We find ourselves telling each other the deepest details of our lives..
Things we don't even shares with our families who raised us .......


But what is a friend??
A confidant?
A lover?
A follow email junkie?
A shoulder to cry on?
An Ear to listen?
A heart to feel?


A friend is all these things and more
No matter where we met,......
I call you friend.


A world so small... yet so large in feeling....
A word filled with emotion.


It is true great things come in small packages.
Once a package of friendship has been opened, it can never be closed.
it is constant book always written waiting to be read and enjoyed.




we may have our disagreements.....
we may argue...
we may concern one another......
A friendship is a Unique bond that lasts through it all....


A part of me is put into my friends...
some it is my Humor.....
some it is my listening ear......
some it is real life experiences...
some it is my romanticims
but will all, it's FRIENDSHIP.


We have been friends for such a long time and lovely time.
There is no friend like the old friend who has shared our morning days
No greeting like his welcome.
No homage like his Praise,
Fame is the scentless sunflower, with a gaudy crown of Gold
But friendship is the breathing, nose with sweat is every fold

THANKS FOR BEING A VERY GOOD FRIENDS TO ME.

Tuesday, November 22, 2011

Chadema kumwona Rais Kikwete Ikulu


Written by  //  22/11/2011  //  Habari  //  2 Comments
Na Muhibu Said
22nd November 2011
-Ni kamati ya wajumbe saba
-Kuwasilisha ujumbe mzito

Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), imeunda kamati ndogo inayoundwa na vigogo saba, wakiongozwa na Mwenyekiti Taifa, Freeman Mbowe, kwa ajili ya kwenda kuzungumza na Rais Jakaya Kikwete, kuhusiana na msimamo wa chama hicho juu ya kuboresha mchakato wa kupata Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Vigogo wengine wa Chadema wanaounda kamati hiyo, ni Katibu Mkuu, Dk. Willibrod Slaa; Makamu Mwenyekiti Tanzania Bara, Said Amour Arfi; Makamu Mwenyekiti Zanzibar, Said Issa Mohammed; wajumbe ni wa Kamati Kuu ya Chadema, Profesa Mwesiga Baregu, Profesa Abdallah Safari na Tundu Lissu, ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki na Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.
Hatua ya kuundwa kwa kamati hiyo, ni miongoni mwa maazimio tisa yaliyofikiwa na Kamati Kuu ya Chadema katika kikao chake maalum, kilichofanyika Jumapili ya wiki iliyopita, jijini Dar es Salaam.
Pamoja na mambo mengine, kikao hicho kilipokea na kujadili kwa kina taarifa ya majadiliano na kupitishwa na Bunge kwa Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011 na hatua za kuchukua.
Maazimio hayo yalisomwa na Mbowe alipozungumza na waandishi wa habari makao makuu ya Chadema, jijini Dar es Salaam jana.
Akisoma maazimio hayo, Mbowe, ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, alisema mazungumzo kati ya kamati hiyo na Rais Kikwete, yanalenga kutaka kumpa msimamo, mawazo na ushauri wao namna ya kuuboresha mchakato huo.
“(Rais Kikwete) akisikiliza mawazo yetu, tutashiriki mchakato (wa kuandika Katiba mpya), akikataa tutakwenda kwa wananchi,” alisema Mbowe, ambaye pia ni Mbunge wa Hai.
Alisema Kamati Kuu inaamini kuwa pamoja na sheria hiyo kupitishwa, bado kuna fursa za kisiasa na kijamii katika kujenga mwafaka wa kitaifa juu ya haja, nia, mchakato na misingi ya Katiba mpya.
Hata hivyo, alisema Kamati Kuu imeshangazwa na kusikitishwa na uamuzi wa Rais Kikwete wa kutozitumia fursa hizo na badala yake kujiingiza katika kile alichokiita “Jalala la taka za upotoshaji” uliofanywa na wabunge wa CCM juu ya misingi na maudhui ya sheria hiyo.
Alisema Kamati Kuu inaamini kwamba, badala ya kuwaunganisha Watanzania na kujenga mwafaka unaohitajika katika mchakato wa Katiba mpya, hotuba ya Rais Kikwete kwa wazee wa CCM wa Mkoa wa Dar es Salaam ya Ijumaa wiki iliyopita, imezidi kuwagawa Watanzania kwa misingi ya ushabiki wa vyama badala ya kuwaunganisha kwa misingi ya utaifa.
Hata hivyo, Mbowe alisema Chadema itaendelea kutoa elimu kwa wananchi na wadau wote juu ya haja ya kuwa na sheria itakayoweka utaratibu bora zaidi wa kuunda Tume Shirikishi ya Katiba kwa lengo la kukusanya maoni ya wananchi, kuandaa ripoti na rasimu ya Katiba mpya, Bunge Maalum la Katiba na usimamizi wa kura ya maoni itakayowezesha wananchi kufanya maamuzi kwa uhuru na kwa haki.
Alisema ushiriki wa Chadema katika mchakato wa kupata katiba mpya uliowekwa na sheria hiyo, utategemea utayari wa serikali kufanya mabadiliko makubwa na ya kimsingi katika sheria hiyo kwa lengo la kujenga muafaka wa kitaifa juu ya mchakato huo.
Akijibu swali lini wanatarajia kukutana na Rais Kikwete, Mbowe alisema: “Haraka iwezekanavyo” na kwamba, mchakato kuhusu suala hilo unaoshughulikiwa na kamati nyingine ya ufundi ya chama hicho, ulianza rasmi jana.
Kabla ya Mbowe kusoma maazimio hayo, Lissu alianza kwa kuelezea sababu zilizowafanya wabunge wa Chadema kususia mjadala na upitishwaji wa muswada huo bungeni, kinyume cha baadhi ya watu wanavyopotosha.
Lissu alitaja sababu saba kati ya nane zilizomo katika maazimio ya Kamati Kuu za kususia suala hilo na kusema ya kwanza ni mchakato wa kupitisha muswada huo ndani ya Bunge, kukiuka kanuni za kudumu za Bunge.
Alisema muswada uliosomwa mara ya kwanza bungeni sio ulioletwa bungeni kusomwa mara ya pili na baadae kupitishwa.
Lissu alisema Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala ilizuiliwa kukusanya maoni ya wananchi katika mikoa na maeneo mbalimbali.
Alisema pia Spika wa Bunge, Anne Makinda, aliingilia kazi na majukumu ya kamati hiyo, ikiwa ni pamoja na yeye mwenyewe (Spika) na baadhi ya wajumbe wa CCM, kukusanya maoni nje ya utaratibu wa kamati na baadaye kuingiza wajumbe wengine wa CCM, CUF na NCCR-Mageuzi wa lengo la kupitisha matakwa ya CCM na serikali ndani ya kamati.
Sababu ya pili, alisema ni sheria iliyopitishwa na Bunge kumpa Rais wa Jamhuri ya Muungano, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM mamlaka makubwa ya kuunda Tume ya Katiba na Sekretarieti yake.
Alisema tume hiyo sio tu itakusanya maoni ya wananchi na kuandaa ripoti, bali pia ndiyo itakayoandaa na kuandika rasimu ya katiba mpya na kusimamia mchakato wote wa wananchi kuijadili na kuipitisha katika Bunge la Katiba.
Sababu ya tatu, alisema ni sheria hiyo kumpa Rais mamlaka makubwa sio tu ya kupokea ripoti ya Tume ya Katiba, bali pia ya kuifanyia mabadiliko, ambayo yeye na serikali yake wataona yanafaa kwa kutumia taratibu za kiserikali za kutunga sheria.
Alitaja sababu ya nne kuwa ni sheria hiyo kumpa Rais mamlaka makubwa ya kuliitisha tena Bunge la Katiba kwa lengo la kufanya mabadiliko kwenye katiba mpya endapo litapitisha katiba mpya, ambayo yeye Rais au serikali yake, au chama chake wataona hailindi maslahi yao.
Nyingine ni sheria hiyo kuunda Bunge la Katiba, ambalo litakuwa na wajumbe hadi 400 wa CCM kati ya wajumbe 545 wa Bunge la Katiba.
Lissu alisema idadi hiyo ya wajumbe itaiwezesha CCM kupata theluthi mbili ya wajumbe wanaohitajika chini ya sheria hiyo kupitisha jambo lolote katika Bunge la Katiba na kwa hiyo, akasema Katiba mpya itakuwa ni ile inayolingana na matakwa na maslahi ya CCM na itakuwa mpya kwa jina tu.
Sababu ya sita, alisema ni sheria kutoa nafasi kubwa kwa Rais wa Zanzibar na Makamu Mwenyekiti wa CCM na vyombo vya uwakilishi vya Zanzibar kushiriki kutunga Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano kinyume cha Makubaliano ya Muungano ya Mwaka 1964 na Katiba ya sasa, ambayo imevipa mamlaka ya kutunga katiba ya Jamhuri ya Muungano vyombo vya Muungano kama serikali na Bunge, ambako Zanzibar ina uwakilishi wa kutosha.
Lissu alisema sababu ya saba, ni sheria kuhakikisha kwamba muundo wa sasa wa Muungano wa serikali kutoguswa bali utadumishwa na kutiliwa nguvu licha ya madai ya miaka mingi ya wananchi na mapendekezo ya Tume za Kiserikali kwamba muundo wa Muungano uwe ni wa serikali tatu.
Sababu ya nane, alisema ni sheria kuipa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) iliyoteuliwa na Rais mamlaka ya kusimamia mchakato wa kura ya maoni ya kuipa Katiba mpya uhai wa kisheria.
Alisema NEC haina uhuru na imeshindwa mara nyingi kusimamia chaguzi huru na haki nchini, hivyo, haiwezi kusimamia kura ya maoni kwa uhuru unaohitajika.
SLAA APONGEZA WABUNGE WA CHADEMA KUSUSIA
Baada ya Lissu kueleza hayo, Dk. Slaa naye alitumia fursa hiyo kueleza azimio mojawapo la Kamati Kuu linalowapongeza wabunge wote wa Chadema kwa hatua walizochukua kupinga muswada huo kusomwa kwa mara ya pili na kujadiliwa bungeni bila wananchi kushirikishwa kwa ukamilifu na kutoa maoni yao na muswada huo kuboreshwa kwa kuzingatia muafaka wa kitaifa.
“Kamati Kuu imewapongeza wabunge wa Chadema kwa kususia vikao vya Bunge vilivyojadili na kupitisha sheria hiyo, kwani kushiriki kwao kungeipa uhalali wa kisiasa na kijamii sheria ambayo haikuzingatia nia na haja ya dhati ya kuweka utaratibu wa kisheria utakaoiwezesha nchi yetu kupata Katiba mpya yenye kuzingatia na kukidhi matakwa ya umma wa Watanzania,” alisema Dk. Slaa.
Baada ya Dk. Slaa kueleza azimio hilo, Mbowe alisoma maazimio mengine ya Kamati Kuu, ambayo alisema imezingatia kuwa sheria iliyopitishwa na Bunge ina upungufu mwingi na wa msingi, ambao hautajenga muafaka wa kitaifa juu ya Katiba mpya na hautaleta mabadiliko yoyote ya kimsingi ya Katiba.
Mbowe alisema Kamati Kuu imesisitiza siku zote kwamba, mchakato wa kupata Katiba mpya unahitaji mwafaka wa kitaifa, ambao utazingatia maoni mapana ya makundi mbalimbali ya kijamii.
Alisema Kamati Kuu inasikitishwa na hatua za makusudi za kufifisha juhudi zote zilizofanyiwa na wadau mbalimbali katika kufikia mwafaka wa kitaifa juu ya sheria hiyo.
Mbowe alisema Kamati Kuu pia imesikitishwa na upotoshaji wa makusudi wa hotuba ya Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni uliofanywa na wabunge wa CCM na CUF, wakiongozwa na Spika wa Bunge, Makinda, kuhusu msimamo wa Chadema juu ya Muungano.
Alisema Kamati Kuu inasisitiza kwamba, njia pekee ya kunusuru Muungano ni kwa wananchi wa pande zote mbili kupiga kura ya maoni kuamua kwamba wanataka kuendelea na Muungano na kama jibu ni ndio, muundo gani wa Muungano huo wanaoutaka.
“Kamati Kuu inarudia msimamo wa Chadema kwamba ili kuondoa kero na malalamiko ambayo yameuandama Muungano wetu tangu kuzaliwa kwake, muundo unaofaa ni wa serikali tatu kama ilivyopendekezwa pia na Tume ya Nyalali mwaka 1991 na Tume ya Kisanga mwaka 1998,” alisema Mbowe.
Alisema katika maazimio hayo, Kamati Kuu inawaagiza wabunge na viongozi wote wa chama katika ngazi zote, kufanya mikutano ya ndani na hadhara, yenye lengo la kuwaelimisha wananchi juu ya sheria hiyo na madhara yake kwa mchakato wa kupata Katiba mpya na bora nchini.
Mbowe alisema Kamati Kuu inaamini kwamba uamuzi wa serikali kulitumia Jeshi la Polisi kuzuia mikutano ya hadhara na maandamano ya amani ya wananchi wanaopinga mchakato uliopitishwa kuwa sheria, si tu ni kwenda kinyume cha haki za kimsingi za Kikatiba, bali pia unahatarisha moja kwa moja amani, utulivu na umoja nchini.
“Kamati Kuu inasikitishwa na msimamo huu wa serikali ya CCM kwani unashindwa kutambua ukweli kuwa matumizi ya nguvu za dola hayajawahi kuokoa serikali … na katiba mpya kupatikana katika nchi mbalimbali duniani na katika Bara la Afrika,” alisema Mbowe.
Alisema ni unyanyasaji mkubwa kwa polisi kuizuia Chadema, lakini wabunge wa CCM wakiruhusiwa kwenda mikoani kutoa elimu ya sheria hiyo.
Alisema Kamati Kuu inasisitiza kwamba Chadema itaendelea kutumia njia zote za amani, ikiwamo mikutano ya hadhara na maandamano kama ilivyoanishwa na Katiba na sheria husika za nchi kupinga sheria ya mabadiliko ya katiba na mchakato wake utakaopelekea Tanzania kutopata Katiba mpya na ubora.
CHANZO: NIPASHE

Sunday, November 20, 2011

FIRST WORLD

To reflect and ...............Act.
The difference between poor country and the rich ones is not age of the country.

This can be shown by countries like India $ Egypt, that are more than 2000 years old and are poor.

On the other hand, Canada, Australia $ New Zealand, that 150 years ago were inexpressive, today are developed countries and are rich.

The difference between poor and rich countries does not reside in the available natural resources.

Japan has limited territory, 80% mountainous, in adequate for agriculture $ cattle raising, but it is the third world economy. The country is like an immense floating factory, importing raw material from the whole world and exporting manufactured products.

Another example is Switzerland, which does not plant cocoa but has the best chocolate of the world. in it little territory they raised animals and plant the soil during 4 mounths  per year. Not enough, they produce dairy products of the best quality. It is a small country  that transmits an image of security, order $ labor, which made it the world's strong safe.

Executives from rich countries who communicate with their counterpart in poor countries show that there is no significant intellectual difference.
Race or skin colour  are also not important:- Immigrants labeled lazy in their countries of origin are the productive power in rich European countries.

                          what is the difference then?
  • The difference is the altitude of the people, framed  along the years by the Education $ the culture.
  • On analyzing the behavior of the people in rich $ developed countries, we find that the great majority follow the following principles in their lives:-
  1. Ethics, as a basic principles.
  2. Integrity
  3. Responsibility.
  4. Respect to the law $ rules.
  5. Respect to the rights of citizens.
  6. Work loving.
  7. Strive for saving $ Investment.
  8. Will of super action.
  9. Punctuality.
In poor countries only a minority follow these basic principles in their daily life. 
We are not poor because we lack natural resources or because nature was cruel to us.
We are poor because we lack altitude.
We lack the will to comply with and teach functional principal of rich $ developed societies.

IF YOU LOVE YOUR COUNTRY, LET THIS MESSAGE CIRCULATE FOR A MAJOR QUANTITY OF PEOPLE COULD REFLECT ABOUT THIS CHANGE... ACT!!


Saturday, November 19, 2011

I HOT MY MOM

My mom only had one eye.
MY MOM.

I hated her............ she was such an embarrassment.
she cooked for students $ teachers to support the family.
There was this one day during elementary school where my mom come to say hello to me.
I was so embarrassed.
How could she do this to me?
I ignored her, threw her a hateful look and ran out.


The next day at the school one of my classmates said,
"EEEE,  your mom only has one eye!"
I wanted to bury myself, I also wanted my mom to just disappear.
so I confronted her that day and said,
"if you're only gonna make me a laughing stock, why don't you just die?!!!"
My mom did not respond...................................
I didn't even stop to think for a second about what I had said, because I was full of anger.
I was obvious to her feelings, I wanted out of that house, and have nothing.
so I study real hard got a chance to go to Singapore to study.


Then, I got married.
I bought a house of my own,

I had kids of my own.
I was happy with my life, my kids and the comforts.
Then one day, my mother came to visit me. she hadn't seen me in years and she didn't even meet her grandchildren.
When she stood by the door, my children laughed at her, and I yelled at her for coming over uninvited.
I screamed at her, 
"How dare you came to my house and scare my children!!"
GET OUT OF HERE!  NOW!!!!
and to this my mother quietly answered, 
oh I'm so sorry. I may have gotten the wrong address, and she disappeared out of sight,


One day, a letter regarding a school reunion came to my house in Singapore.
So I lied to my wife that I was going on a business trip.
After reunion, I went to the old shack just out of curiosity.
My neighbors said that "she died".
I did not shed a single tear.
They hand me a letter, that she had wanted me to have.


"My dearest son, I think of you all the time.
I'm sorry that I came to Singapore and scared you children.
I so glad when I heared you were coming for the reunion.
But I may not be able to even get out of bed to see you.


I'm sorry that I was a constant embarrassment to you when you were growing up.


You see........................ when you were very little, you got into an accident, and lost your eye.

As a mother, I couldn't stand watching you having to grow up with one eye.
so I gave you mine.
I was so proud of my son who was seeing a whole new world for me, in my place, with that eye.
                                           With my love to you,
                                                YOU MOTHER.



Hotuba ya Raisi Kikwete Kwa wazee wa Jiji la Dar Es Salaam 18/11/11


HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA

TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, 

KWA WANANCHI KUHUSU HALI YA UCHUMI NCHINI NA MCHAKATO WA KATIBA MPYA, TAREHE 17 NOVEMBA, 2011

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa,
Mstahiki Meya,
Viongozi wa Serikali,
Wazee wangu,
Ndugu Wananchi,

Nakushukuru Mkuu wa Mkoa na viongozi wenzako wa Jiji la Dar es Salaam kwa kuniandalia fursa hii ya kukutana na Wazee wa Dar es Salaam. Nawashukuru sana wazee wangu kwa kuitikia wito wangu huu wa kukutana nanyi. Nimefarijika sana kwa mahudhurio yenu makubwa pamoja na taarifa kuwa ya muda mfupi.
Nimewaiteni wazee wangu nizungumze nanyi na kupitia kwenu nizungumze na wananchi wote wa Tanzania. Mwisho wa mwezi uliopita sikuweza kufanya hivyo kupitia utaratibu wetu wa kawaida kwa sababu nilikuwa kwenye Mkutano wa Jumuiya ya Madola nchini Australia. Mwisho wa Mwezi huu nitakuwa Bujumbura kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, hivyo sitaweza kuongea na wananchi wakati huo. Lakini, yapo masuala kadhaa ambayo ni muhimu watu kupata ufafanuzi kutoka kwangu. Kwa ajili hiyo nimeona nitumie fursa hii kuzungumza nanyi siku ya leo. Leo nataka kuzungumzia hali ya uchumi na mchakato wa kupata Katiba Mpya.


Raisi  wa jamuhri ya muungano wa Tanzania.: Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.



Hali ya Uchumi
Ndugu Wananchi;
Katika kuelezea hali uchumi nchini, naomba nianze kwa kuelezea hali ya uchumi duniani kwani yanayotokea nchini yana uhusiano mkubwa na yanayotokea duniani. Hali ya uchumi duniani siyo shwari. Ukweli ni kwamba hali katika uchumi wa mataifa ya Marekani, Ulaya Magharibi na Japan haijatengemaa kufuatia machafuko ya masoko ya fedha na mdororo wa uchumi wa miaka miwili iliyopita. Hivi sasa uchumi wa mataifa tajiri ya Ulaya , wanachama wa Umoja wa Ulaya na hasa wanachama wa Umoja wa Sarafu ya Euro unapita katika kipindi kigumu na mashaka. Thamani ya sarafu hiyo inashuka na hata kuaminika kwake ni kwa mashaka. Mfumuko wa bei umepanda, ukosefu wa ajira umeongezeka na ipo hofu kubwa ya uchumi wa nchi hizo kudorora tena. Lakini nchi hizi ndiyo masoko makubwa ya bidhaa zetu, watalii na bidhaa za viwandani. Hivyo, athari zao zinatugusa na sisi. Kuongezeka kwa mfumuko wa bei kunaongeza bei ya bidhaa tunazonunua kutoka kwao. Aidha, kutetereka kwa uchumi wao nako kumepunguza masoko ya bidhaa zetu. 

Lakini kulegalega kwa sarafu ya Euro kumesaidia kuimarika kwa sarafu ya dola ambayo kabla ya hapo ilikuwa imepungua nguvu. Kwa sababu hiyo thamani ya sarafu ya dola imepanda duniani ikilinganishwa karibu na sarafu nyingine zote pamoja na yetu. Wakati huo huo bei ya mafuta imeendelea kupanda duniani kutoka dola 76.1 kwa pipa Septemba,, 2010 hadi dola 100.5 Septemba, 2011. Jumla ya yote haya ni kuongezeka kwa mfumuko wa bei kutoka asilimia 4.2 Oktoba, 2010 hadi asilimia 17.9 Oktoba, 2011.

Ndugu Wananchi;
Serikali na vyombo husika vimekuwa vinachukua hatua mbalimbali kukabiliana na matatizo ya kushuka kwa thamani ya shilingi, bei ya mafuta, bei ya sukari na matatizo ya umeme. Kuhusu kushuka kwa thamani ya shilingi Benki Kuu imeendelea kuchukua hatua zilizopo ndani ya mamlaka yake hususan kubana ulanguzi wa fedha za kigeni, kudhibiti matumizi ya fedha kigeni kufanyia malipo hapa nchini na kuongeza fedha za kigeni katika masoko ya fedha. Kwa kweli uwezo wao una ukomo. Jawabu la uhakika lipo kwenye uchumi wa mataifa makubwa kuchukua hatua thabiti kuimarisha uchumi wao ili thamani ya dola irejee mahali pake stahiki na bidhaa zetu zipate masoko ya uhakika na bei nzuri ili mapato yetu ya fedha za kigeni yaongezeke.

Kwa upande wa mfumuko wa bei, ni vyema tukatambua kuwa Asilimia 75 ya ongezeko hili imetokana na kupanda kwa bei ya chakula na mafuta. Asilimia 25 iliyobaki imechangiwa na sera za fedha. Kwa upande wa mafuta, tunaamini utaratibu wa kuagiza mafuta kwa pamoja utasaidia kudhibiti bei za ndani za bidhaa hiyo. Aidha, itsaidia kupunguza makali ya athari ya bei za dunia zinazopanda. Kwa upande wa bei za vyakula, tatizo kubwa ni uhaba wa chakula katika nchi jirani unaosababisha wote kututegema sisi na hivyo kupandisha bei nchini. Tunaendelea kudhibiti magendo ya chakula na wakati huo kutengeneza taratibu rasmi za kuziuzia chakula nchi jirani.
Kwa upande wa sukari tumeamua kuruhusu tani 120,000 ziagizwe ili kupunguza uhaba wa bidhaa hiyo na kushusha bei yake.


Hatuko Peke Yetu
Ndugu Wananchi;
Ni vizuri tukafahamu kuwa, matatizo ya mfumuko wa bei na kushuka kwa thamani ya fedha yetu siyo yetu peke yetu. Nchi zote za Afrika Mashariki zinakabiliana na matatizo haya. Kwa mfano, mfumuko wa bei kwetu ni asilimia 17.9, Kenya wako asilimia 18.9 na Uganda asilimia 30.5. Wakati mwaka wa jana sote tulikuwa kwa watani karibu asilimia 5. Kwa upande wa kushuka kwa thamani ya shilingi dhidi ya dola sote tumeathirika. Shilingi ya Tanzania imeshuka kwa asilimia 9.4, Kenya kwa asilimia 6.8 na Uganda kwa asilimia 17.4. Randi ya Afrika Kusini kwa asilimia 18.7, Rupia ya India kwa asilimia 9.8, Pauni ya Uingereza kwa asilimia 6.6. na Euro kwa asilimia 9.7. 

Ndugu Wananchi;
Katika kukabiliana na tatizo la umeme, Serikali inaendelea kutekeleza mpango wa dharura wa kuongeza uzalishaji wa umeme. Serikali imewawezesha TANESCO kukodi mitambo ya kuzalisha umeme kutoka kwenye makampuni ya Symbion (112 MW) na Aggreko (100 MW) na kununua mafuta ya kuendeshea mitambo ya IPTL (100 MW).
Napenda niwahakikishie wananchi kuwa, ifikapo Desemba, 2011 hali ya upatikanaji wa umeme itakuwa nzuri na mgao utapungua sana baada ya kufunga mitambo mingine mipya ya kuzalisha umeme ya TANESCO (160 MW) na Symbion (60 MW). Mikakati tuliyonayo ya muda mrefu ni kuongeza mitambo zaidi na kuongeza upatikanaji wa gesi ya kuendeshea mitambo kwa kujenga bomba kubwa la gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam.

Mchakato wa Katiba
Ndugu Wananchi;
Kama mtakavyokumbuka tarehe 31 Desemba 2010 katika hotuba yangu ya kuuaga mwaka 2010 na kuukaribisha mwaka 2011 nilizungumzia maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika ambayo sasa ni Tanzania Bara tarehe 9 Desemba, 2011. Miongoni mwa mambo ambayo niliyataja kuwa tutayafanya katika kusherehekea siku hiyo adhimu ilikuwa ni kuanzisha mchakato wa kuitazama upya Katiba ya nchi yetu kwa nia ya kuihuisha ili hatimaye tuwe na Katiba mpya.
Nilifafanua siku ile kwamba tunataka kufanya hivyo si kwa sababu Katiba yetu ya sasa ni mbaya, la hasha! Nilieleza kwamba Katiba yetu ya sasa ni nzuri na imelilea vyema taifa letu. Tuna nchi yenye amani, utulivu na umoja pamoja na watu wake kuwa wa rangi, makabila, dini na itikadi mbalimbali za kisiasa. Tunayo nchi ambayo imepiga hatua kubwa sana ya maendeleo ukilinganisha na ilivyokuwa miaka 50 iliyopita. Pamoja na hayo tunataka kuihuisha Katiba yetu ili tuwe na Katiba inayoendana na Tanzania ya miaka 50 baada ya Uhuru wa Tanzania Bara, Tanzania ya miaka 47 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar na Tanzania ya miaka 47 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Kwa ajili hiyo nilielezea dhamira yangu ya kuunda Tume Maalum ya Katiba yaani Constitutional Review Commissionitakayojumuisha Watanzania wa makundi mbalimbali katika jamii yetu na kutoka pande zetu mbili za Muungano. Aidha, nilifafanua kuwa jukumu la msingi la Tume hiyo litakuwa ni kuongoza na kuratibu mchakato wa kupata maoni ya Watanzania kuhusu nini wanachokitaka kiwemo katika Katiba yao. 

Tume itasikiliza maoni hayo na baadaye kutengeneza rasimu ya Katiba mpya ambayo baada ya kukubaliwa na Bunge itafikishwa kwa wananchi kutoa ridhaa yao kwa kupiga kura. Nilisisitiza kuwa mchakato huo utawahusisha Watanzania wote wa ngazi zote na popote walipo mijini na vijijini. Hapatakuwa na aina yoyote ya kuwabagua watu kwa itikadi zao za siasa, shughuli wazifanyazo, dini zao, rangi zao au jinsia zao.

Ndugu Wananchi;
Nilifarijika sana na kauli za pongezi kwangu na kwa Serikali kwa uamuzi wa kuanzisha mchakato wa kupata Katiba mpya. Miongoni mwa waliotoa pongezi alikuwa Ndugu Freeman Mbowe, Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa CHADEMA ambaye wakati akichangia hotuba yangu ya kufungua Bunge Jipya, tarehe 11 Februari, 2011; nanukuu Hansad ya Bunge aliposema “Mheshimiwa Spika, ninapenda kwenye hili, nimpongeze Rais kwa kuwa msikivu, na Rais anapofanya jema tutampongeza, Serikali yake inapofanya jema tutaipongeza na Chama chochote kitakapofanya jambo jema kwa Taifa letu, tutakipongeza. Napenda kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa sababu moja ya msingi sana, kuridhia mabadiliko au kuitafuta upya Katiba ya nchi yetu.” mwisho wa kunukuu. Lakini siku chache baadaye Chama chake kikaja na msimamo tofauti, wakawa wanalalamikia kunyang’anywa hoja yao na kukataa Rais asiunde Tume ya Katiba na wala asihusike kabisa na mchakato huu. Tangu wakati huo wameendesha kampeni kubwa ya kutaka Rais asihusishwe kwenye.

Wazee wakiwa makini kumsikiliza Mhe Kikwete.     


mchakato wa kubadili KatibaKwa kweli watu wengi wanaoitakia mema nchi yetu walishangazwa na madai hayo na vitendo vya ndugu zetu hao. Hii si mara ya kwanza kwa nchi yetu kufanya zoezi la marekebisho ya Katiba au hata kuandika upya Katiba tangu Uhuru na Muungano. Mara zote hizo iliundwa Tume ya kukusanya maoni ya wananchi ambayo iliundwa na Rais. Ndivyo ilivyokuwa wakati wa Rais wa Kwanza, Mwalimu Julius Nyerere, Rais wa Pili, Mzee Ali Hassan Mwinyi na Rais wa tatu Mzee Benjamin Mkapa. Mwalimu Julius Nyerere alifanya hivyo mara tatu. Mara ya kwanza mwaka 1963 wakati wa kubadilisha mfumo wa vyama vingi kwenda Chama kimoja, Rais aliunda Tume ya Mheshimiwa Rashid Kawawa, Amon Nsekela. Mara ya pili wakati wa kutengeneza Katiba ya Kudumu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 aliunda Tume ya Mzee Sheikh Thabit Kombo. 

Mwaka 1984 Mabadiliko ya Katiba ya 1977 yaliyoweka ukomo wa Urais na kuingiza katika Katiba Haki za Binadamu, yaliyotokana na mchakato uliokuwa ni wa Kichama, ambapo CCM ilikusanya maoni kupitia mtandao wa kichama kuanzia Matawi hadi kufikia Makao Makuu. Wakati wa Rais Ali Hassan Mwinyi wa Awamu ya Pili, kulikuwa na Tume ya Jaji Mkuu Francis Nyalali iliyotuletea mabadiliko ya nane ya Katiba yaliyoruhusu vyama vingi vya siasa. Wakati wa Rais wa Awamu ya Tatu, mzee Benjamin Mkapa kuliundwa Tume ya Jaji Kisanga iliyoleta mabadiliko ya 13 na 14 ya Katiba ya nchi.
Hivyo la ajabu lipi kwa Rais wa sasa kuunda Tume ya Katiba? Amepungukiwa nini Kikatiba na Kisheria ambacho Marais wenzake walikuwa nacho katika madaraka yao? Hakipo hata kimoja! Madaraka waliyokuwa nayo Marais waliomtangulia ndiyo aliyonayo Rais wa sasa. Hajapungukiwa chochote kwa mujibu wa Katiba na Sheria za nchi. Kwa kweli hakuna hoja yoyote ya msingi ya kumuengua Rais katika mchakato wa kutengeneza Katiba ya nchi. Haipo hoja ya Kikatiba wala ya Kisheria. Hivi Rais asipounda Tume, nani aiunde Tume hiyo? Na huyo atakayeunda atapatikanaje?

Juzi Bungeni msemaji wa kambi ya upinzani, katika mjadala wa Muswada wa Kuunda Tume ya Kukusanya Maonialisema Rais ni dikteta. Ama kweli “akutukanae hakuchagulii tusi” kama ulivyo msemo wa Kiswahili. Hivi mimi kweli ni dikteta? Kwa jambo lipi? Hivi ndugu zangu Rais dikteta anatoa uhuru mkubwa kama uliopo sasa wa vyombo vya habari na wa watu kutoa maoni yao? Kama mimi ningekuwa dikteta kweli nina hakika hata yeye asingethubutu kusema hivyo na kama angethubutu basi mpaka sasa asingekuwa anatembea kwa uhuru. Mimi ninachofahamu ni kuwa nasemwa kwa kuwapa watu, vyama vya siasa na vyombo vya habari uhuru mkubwa mno ambao watu wanaona unatumika vibaya kusema maneno yasiyokuwa na staha au hata matusi, fitina na kupandikiza chuki katika jamii. Labda, nijaribu kuwa dikteta kidogo watu waone tofauti yake. Naamini kungekuwa na malalamiko makubwa zaidi ya haya.

Ndugu Wananchi;
Mimi na wenzangu Serikalini tumefanya yote ambayo Katiba ya nchi na Sheria vinaruhusu. Ndivyo Marais walionitangulia na Serikali zao walivyofanya tena sisi tumefanya zaidi ya wao. Wote waliunda Tume za kukusanya maoni ya Katiba na wakati wa Mwalimu Julius Nyerere liliundwa Bunge Maalum la Katiba lililojumuisha Wabunge na wananchi wengine kama tulivyoamua kufanya sisi. Ilifanyika hivyo wakati wa kutengeneza Katiba ya Tanganyika kuwa Jamhuri na Katiba ya Kudumu ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977. Sisi tulichofanya cha ziada ni kulihusisha Bunge kutunga Sheria ya Kuunda Tume ya kusimamia mchakato wa Katiba mpya na vile vile kuwapa wananchi wote ridhaa ya kuamua kwa kuipigia kura Katiba inayopendekezwa. Ni kutokana na nyongeza hii ndipo tukaona busara ya kuwepo kwa Sheria maalum ya kuongoza mchakato wa kupata Katiba mpya. Tumepanua demokrasia na kuwahusisha wananchi wenyewe siyo tu katika kutoa maoni bali pia kutoa uamuzi wa mwisho kuhusu Katiba ya nchi yao, badala ya kuwaachia Wabunge na viongozi wengine Serikalini peke yao. Kwa kweli tunastahili pongezi badala ya shutuma na lawama zisizokuwa na msingi.

Pia inasikitisha kuona au kuwasikia watu wanaojua wakijifanya ukweli huu hawaoni au hawajui. Baya zaidi ni pale wanapojihusisha na kupotosha ukweli na kuipaka sura isiyokuwa ya kweli kuhusu kinachofanywa na Serikali. Mimi hujiuliza kwa nini wanafanya hivi. Kwa nini wanafanya hiyana ya upotoshaji wote huu? Kwa kweli sipati majibu ya uhakika. Labda ndiyo ile dhamira ya kutaka nchi isitawalike. Au ndiyo pengine ni ile nia ya kutaka kwenda Ikulu kwa njia ya mkato. Ati kwa kutumia nguvu ya umma. Basi hata hiyo nguvu unaitumia bila ya kuwa na hoja za kweli? 

Ndugu Wananchi;
Nayasema haya kwa sababu kumekuwepo na upotoshaji mkubwa wa jambo hili tangu baada ya hotuba yangu ya tarehe 31 Desemba, 2010 mpaka wakati wa kuwasilishwa kwa Muswada wa Sheria wa Kuunda Tume ya Mabadiliko ya Katiba uliomalizika leo Bungeni. Upotoshaji wa kwanza ulikuwa ni ule wa kujenga dhana kana kwamba Serikali imewasilisha Muswada wenyewe wa Katiba mpya. Wapo watu wamefanywa waamini hivyo wakati si kweli hata kidogo. Huu ni Muswada ambao ukipitishwa, itaundwa Tume ya kukusanya maoni ya wananchi kuhusu nini wanachokitaka kijumuishwe katika Katiba yao mpya. Kwa maneno mengine, maoni yenu mtakayoyatoa wananchi kwa Tume ndiyo yatakayotumika kutengeneza Katiba mpya.

Ndugu Wananchi;
Katika Muswada huu kuna mambo tuliyotaja kuwa ni ya msingi ambayo yamewekewa wigo wa kuhakikisha yanalindwa. Mambo hayo ni yale ambayo yanalitambulisha taifa letu na tunu zake kuu. Mambo yenyewe ni haya yafuatayo: Kuwepo kwa nchi yetu na mipaka yake; kuwepo kwa Serikali, Bunge na Mahakama; kuwepo kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; kuwepo kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar; umoja wetu, mshikamano wetu na usalama wetu; Mfumo wa uchaguzi kwa kura unaotoa fursa kwa wote; Hifadhi ya haki za Binadamu; Haki za watu; Usawa mbele ya sheria na haki; Uhuru wa kuabudu na kuvumiliana kwa imani zetu. 

Kumekuwepo na upotoshaji ati huko ni kuwaziba watu midomo. Siyo hivyo hata kidogo. Mambo hayo yanajadiliwa, lakini siyo kwa nia ya kuyaondoa bali kuboresha. Kwa mfano, kuhusu Muungano, tunachosema ni kwamba hatujadili kuwepo au kutokuwepo kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, bali namna bora ya kuendesha shughuli za Muungano wetu. Lakini, tulichokifanya siyo kitu kigeni, hata Rais wa kwanza alifanya hivyo mwaka 1963 alipounda Tume ya Mfumo wa Chama Kimoja cha Siasa iliyoongozwa na Mheshimiwa Rashid Kawawa. Alitoa mwongozo na aliyataja mambo ya kulinda. Sisi tulichokifanya ni kuyataja kwenye sheria badala ya kuwa Mwongozo wa Rais.
Ndugu Zangu, Watanzania Wenzangu;

Kwani Katiba ya Nchi ni kitu gani. Katiba hutaja nchi na mipaka yake. Kwetu sisi nchi yenyewe ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayotokana na kuungana kwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na Jamhuri ya Tanganyika. Pili, Katiba inaelezea jinsi nchi hiyo itakavyoendeshwa kwa maana ya mihimili mikuu mitatu ya dola ya Utawala/Serikali, Bunge na Mahakama. Katiba inafafanua jinsi Serikali inavyopatikana, muundo wake na inavyofanya kazi.
Aidha, inaeleza jinsi Bunge linavyopatikana, jinsi linavyofanya kazi ya kutunga sheria na mahusiano yake na mihimili mingine. Vile vile, Katiba inaeleza jinsi Mahakama inavyofanya kazi ya kutoa haki, muundo wake na jinsi Majaji na Mahakimu wanavyofanya kazi. Kwa kweli mchakato wote huu unahusu hayo. Tunatakiwa kutoa maoni juu ya namna gani bora zaidi na ikiwezekana namna mpya ya kuendesha shughuli za Muungano wetu na jinsi mihimili yetu inavyopatikana na kufanya shughuli zake.

Ndugu Wananchi;
Jambo lingine lililopotoshwa ni dhana ya muswada kusomwa mara ya kwanza. Kwa mujibu wa utaratibu wa kutunga sheria, Miswada, husomwa mara tatu Bungeni. Muswada kusomwa mara ya kwanza ni pale unapogawiwa kwa Wabunge baada ya kuchapishwa katika gazeti la Serikali siku 21 kabla ya kuwasilishwa Bungeni. Baada ya kuchapishwa, hugawiwa kwa Wabunge. Muswada husomwa mara ya kwanza Bungeni ili kutoa fursa kwa Mheshimiwa Spika kuwasilisha Muswada huo kwenye Kamati iuchunguze na kuutolea maoni. Mheshimiwa Spika anaweza pia kuielekeza Kamati kutafuta maoni ya wananchi. 

Baada ya Kamati kukamilisha kazi yake, Muswada husomwa mara ya pilli ambapo Muwasilishaji atatoa hoja kwamba Bunge liujadili Muswada pamoja na kutoa maelezo ya Muswada. Mjadala huanza kwa Kamati ya Bunge kutoa maoni yake ikifuatiwa na maoni ya Kambi ya Upinzani. Wakati Kamati ya Bunge inapojadili Muswada, Waziri mhusika huwepo na mara nyingi maoni ya Kamati ya Wabunge na wadau hujumuishwa wakati Waziri anapowasilisha hoja Bungeni ya Muswada unaposomwa mara ya pili. Baada ya mjadala, Bunge hukaa kama Kamati ya Bunge zima ambapo hupitia Muswada kifungu kwa kifungu. 

Katika hatua hii Wabunge huweza kupendekeza mabadiliko mahsusi kwenye kila kifungu. Aidha, Waziri nae anaweza kutetea marekebisho ya Muswada. Baadaye Bunge hurejea, taarifa ya Kamati ya Bunge zima hutolewa kwamba Muswada umepitiwa kifungu kwa kifungu na kukubaliwa. Kisha Muswada husomwa mara ya tatu kuashiria kwamba Muswada umepitishwa. Mara nyingi Muswada hutokana na majadiliano katika hatua hizi zote, mabadiliko hufanywa na wakati mwingine mabadiliko huwa makubwa kiasi kwamba kufanya Muswada uliochapishwa na kusomwa mara ya kwanza na ule uliokubaliwa mwishoni uwe tofauti kabisa.

Ndugu Wananchi;
Muswada huu ulisomwa mara ya kwanza mwezi Aprili na kupelekwa kwenye Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala mwezi Aprili, 2011. Tangu wakati huo Kamati imekuwa ikiufanyia uchunguzi Muswada huo na kukusanya maoni ya wadau. Walisikiliza wadau Dodoma, Dar es Salaam na Zanzibar pamoja na kufuatilia maoni ya makongamano, magazetini na kwenye mitandao. Kisha Kamati ikayajadili na kutoa mapendekezo yake ambayo Serikali iliyasikiliza na kuyajumuisha wakati uliposomwa mara ya pili. Muswada huu haukuwahi kuondolewa Bungeni. Kwa sababu hiyo, hakuna sababu ya kurudia kusomwa mara ya kwanza kwa mujibu wa taratibu za kuendesha Bunge.
Tukumbuke kwamba baadhi yao waliahidi kwamba wangetoa Katiba Mpya katika siku mia moja tu. Serikali imechukua miezi kumi na mmoja na wanalaumu kwamba eti inawahisha mchakato!! Hiyo Katiba ya siku mia moja sijui wangeipataje bila kuwashirikisha wananchi?

Ndugu Wananchi;
Ni kutokana na hoja hizo Spika akaamua Muswada uendelee kujadiliwa na Bunge na leo Bunge limeupitisha Muswada huo. Baadae Muswada utaletwa kwangu kwa ajili ya kutiwa saini uwe Sheria. Baada ya hapo itabakia kazi yangu na Rais wa Zanzibar kuunda hiyo Tume ili mapema mwakani kazi ya kukusanya maoni ya wananchi ianze. Lengo letu ni kuwa ifikapo mwaka 2014 zoezi zima liwe limekamilika ili mwaka 2015 tufanye uchaguzi tukiwa na Katiba mpya. Itapendeza tukisherehekea miaka 50 ya Muungano na Katiba mpya. Ni matumaini yangu kwamba wananchi wote watashiriki kwa ukamilifu kutoa maoni yao kwa Tume hiyo. 


waandishi wakimsikiliza Mhe Kikwete.


Ndugu Wananchi;
Nimechukua muda wenu mwingi kuyafafanua masuala haya kwa umuhimu wake. Nia ni kutaka watu waelewe maoni ya upande wa Serikali. Matatizo ya kiuchumi yanayotukabili tunaendelea kuyashughulikia. Yale yaliyo kwenye uwezo wetu tutayamaliza na yale yaliyo nje ya uwezo wetu tutaendelea kuchukua hatua za kupunguza makali. Aidha, tutaendelea kutoa wito kwa mataifa husika kuchukua hatua thabiti kutatua matatizo yao kwani tunaoumia ni wengi.

Ndugu Wananchi;
Kwa upande wa mchakato wa kupata Katiba mpya nawasihi Watanzania tujiandae kwa maoni ya kutoa kwenye Tume ya Katiba mara itakapoanza kazi. Kwa wale ambao hawatapata walichokitaka nawaomba warudi kundini, sote tuungane kwa hatua inayofuata. Najua wanayo maoni mengi mazuri wayatayarishe na kuyawasilisha kwa Tume itakayoundwa. Njia ya maandamano na vurugu si ya busara kufuata. Haijengi bali inabomoa, haina faida bali hasara nyingi, haina faraja bali machungu kwa pande zote. Busara ituongoze sote kuchagua njia inayojenga, yenye faida, furaha na faraja kwa wote. Tutofautiane bila kupigana. Serikali itaendelea kutekeleza wajibu wake wa kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa nchi ya amani na utulivu.

Mwisho

Ndugu Wananchi,
Naomba nimalizie kwa kuwashukuru wananchi kwa kuwa na subira kwa kipindi chote hiki toka tutangaze nia yetu ya kuanza mchakato wa kupata Katiba mpya. Kwa mara nyingine tena nawaomba mjiandae kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kupata Katiba mpya mara utakapoanza ili tuendelee kuijenga na kuiendeleza nchi yetu na vile vile tuendelee kuithamini na kuitunza amani ya nchi yetu.

Mungu Ibariki Afrika!
Mungu Ibariki Tanzania!
Asanteni sana kwa kunisikiliza!

Wednesday, November 16, 2011

WANAFUNZI WA UDSM WALIOKUWAPO MIKONONI MWAPOLISI WAACHILIWA

Wanafunzi waliokamatwa siku ya ijumaa, katika maandamano yaliofanyika chuo kikuu cha Dar es salaam compus ya mwalimu Nyerere waachiliwa kutoka mikononi mwa polisi.Wanafunzi hao waliokuwa wanaandamana kudai fedha za mikopo za baadhi ya wanafunzi wenzao wa mwaka wa kwanza walikamatwa mara baada ya kukiuka amri ya polisi, iliyowaomba watawanyike kwa madai maandamano hayakuwa halali. walikwekwa ndani kwa muda wa siku takriban tano(5). wameachiliwa leo mara baada ya mgomo wa siku mbili wa kutoingia madarasani.